WANAUCHUMI WAKONGAMANA MOMBASA KWA WARSHA YA SIKU TANO


Jumuiya ya kiuchumi ya kenya( ESK) leo hii wamefungua rasmi warsha itakayochukua  siku tano jijini Mombasa huku dhima ya mwaka huu ikiwa ni  kutoa uongozi kuelekea  katika ukuaji wa uchumi nchini kenya.

Jumuiya hii inayoshirikisha wadau na  wataalamu  mbalimbali kutoka sekta  muhimu za kiuchumi wamekongamana   ili  kutoa fursa  na jukwaa kwa wanauchumi kutoka sekta  mbalimbali  katika kuyajadili  maswala muhimu ya kiuchumi yanayokabili nchi.

Warsha hii imeongozwa na  mkurugenzi
mkuu wa jumuiya  hiyo  Dunstone Ulwodi   ambaye amesema. kwamba  ipo haja kama wanauchumi kuunga mikono  sera za kiuchumi zinazoweza kubadilisha nchi   huku akisisitiza  kwamba sharti  sera za kiuchumi   ziwe sera za kuleta mabadiliko  katika uchumi.

"Tunasema kwamba  sera lazima ziwe  zinabadilisha nchi kwa uzuri,lazima ziwe sera za kuleta mabadilko katika uchumi wa  nchi"

Aidha Mbunge wa Bunge la Afrika mashariki   Suleiman Shabhal  alihudhiria Kongamano hilo  na kusisitiza kwamba  bara la afrika  liko  na mawazo tele katika uwekezaji  lakini   fursa za kuwekeza  katika mawazo hayo ndio  huwa ngumu sababu ya ukosefu  wa kifedha ,Shabhal amesema kwamba ataidhinisha muswada katika bunge la afrika mashariki la (EALA) la  kuweka  benki  ya uwekezaji itakayosaidia  miradi  inayokua  ili kuifanya itekelezwe 

 Aidha amewashauri wanauchumi kuhimiza Sera za Ushirikiano wa Umma na Sekta za  Binafsi (PPP)  ili kuwezesha ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili kuvuta  wawekezaji  wengi akisema hatua hii ya pande zote mbili zinaweza kuleta ufanisi zaidi katika kutoa huduma kwa umma akisema  kwamba  hili halitawezekana kama  wataiachia serikali peke yake  bila kuhuzisha sekta za kibinafsi.

Comments

Popular posts from this blog

Premier Hospital’s Lenah Wangari Karuga Crowned Kenya’s Best Nurse Midwife at NMOYA Awards

SIMBA APPAREL EPZ UNVEILS NEW PRODUCTION FACILITY IN MOMBASA

ABE International Hosts Inaugural Student Entrepreneurship Summit in Mombasa"